Posts

Showing posts from 2018

Mwanamke na Uongozi

Image
Na: RIDHAA KORONGO Miaka ya nyuma nchini Tanzania, wanawake hawakuwa wakipewa kipaumbele katika uongozi. Hata hivyo, hivi karibuni serikali na jamii zimetambua mchango wa wanawake, na hivyo kuanza kuwapa nafasi mbalimbali za uongozi, si tu serikalini bali pia katika taasisi zisizo za kiserikali. Hata hivyo, bado wapo baadhi ya watu wanaoamini kuwa wanawake hawawezi kushika nyadhifa za uongozi kutokana na changamoto wanazokumbana nazo. Wengi wa watu hawa hawajui kuhusu Mtawala wa kike aliyerithi uchifu baada ya baba yake kufariki dunia. Leo, kalamu yangu inawaandikia juu ya Mwami Theresa Ntare VI, aliyezaliwa mwaka 1926 na kufariki mnamo tarehe 23 Mei 1993 akiwa na umri wa miaka 67. Theresa alikuwa mtawala wa kike aliyerithi uchifu baada ya baba yake, Mwami Gwasa, kufariki dunia. Alikabidhiwa uchifu kwa sababu hakuwa na kaka wa kurithi nafasi hiyo katika familia yao. Kinyume na mila zilizotaka kutafutwa mtoto wa kiume kutoka kwa ndugu wengine, Bi. Theresa alipewa nafasi hiyo, na hi...

Tuwalinde watoto wetu na madhara yatokanayo na Pempasi

Image
Na: Ridhaa Korongo Pampasi ya kwanza ilianza kutumika mnamo mwaka 1961 nchini Marekani, baada ya wazo la kutengeneza pampasi kutolewa na Mmarekani Victor Mills mwaka 1956. Hii ilitokana na kuchoshwa kwake na kazi ya kubadili nepi za mjukuu wake. Tangu wakati huo, pampasi zimeenea duniani kote, zikiwapa wazazi njia rahisi zaidi ya kudhibiti haja za watoto. Hapa Tanzania, pampasi zilianza kutumika mapema miaka ya 2000 na zimeendelea kushamiri, hasa katika maeneo ya mijini. Kwa sasa, pampasi zimekuwa sehemu muhimu ya maisha ya wazazi, zikichukua nafasi ya mipira, nepi, na matambara yaliyokuwa yakitumiwa zamani. Wakati huo, kila mzazi alihitaji kuchana vipande vya kanga au kununua nepi kwa ajili ya watoto wao. Lakini siku hizi, imekuwa kawaida kwa kila familia yenye mtoto kuwa na pampasi, ambayo sasa hutumika kama “nguo ya ndani” kwa watoto, ikisaidia kuzuia kinyesi na mkojo kutapakaa. Ingawa pampasi zimewasaidia wazazi kwa kuwaondolea kazi kubwa ya kufua nepi na matambara ma...