Ikiwa ni mwendelezo wa mechi za hatua ya 16 bora Belgium yawafungisha vilago hungary baada ya kupata ushindi mnono wa goli 4-0. Goli la kwanza liliwekwa wavuni na Toby Alberweireld mnamo dakika ya 10 na kuongeza la pili dakika ya 78 kupitia kwake Michy Batshuayi naye Hazard akiwakata maini kwa kufunga la tatu dakika ya 80, hatimaye Carasco akipigilia msumari wa mwisho kwenye jeneza la Hungary dakika za lala salama. Kwa matokeo hayo Belgium watakutana na Wales wanaoongozwa na Gareth Bale na Ramsey Ijumaa hii, mtanange utakaopigwa kwenye dimba la Lille. Mechi nyingine zilizopigwa usiku wa leo ni Ujerumani na Slovakia, Ujerumani wakishinda 3-0, huku Antoine Griezmann akiivusha Ufaransa walioshinda 2-1 dhidi ya Ireland. Ujerumani watakutana na Italy au Spain robo fainali huku Ufaransa kumenyana na England au Iceland Jumapili ijayo.