CLEVELAND CAVALIERS MABINGWA NBA

Lebron James aiongoza Cleveland kubeba ubingwa wa ligi kuu ya kikapu nchini Marekani baada ya
 kupata ushindi wa vikapu 93 kwa 89 vya Golden State Warriors ikiongozwa na mkali Stephen Curry.


Mechi hiyo ambayo ilikuwa ni ya saba kwenye mfululizo wa fainali hizo huku mchuano huo ulikuwa wa kuamua nani anabeba kombe hilo la NBA kila timu ikiwa na ushindi wa mechi tatu.

Lebron James ndiye alikuwa MVP wa mechi hiyo akifunga vikapu 27, assist 11 na rebound 11 huku Kyrie Irving akifunga kikapu cha mwisho cha pointi 3 kilichoipa kombe The cavs.

Lebron ameshinda taji hilo kwa mara ya tatu akijiunga na Michael Jordan ,Bill Russell na Kareem Abdul-Jabbar.



Comments

Popular posts from this blog

Tuwalinde watoto wetu na madhara yatokanayo na Pempasi

Mwanamke na Uongozi

Unyanyasaji wa Kijinsia